JESHI la Polisi nchini Tanzania, limeanza uchunguzi wa picha mjongeo inayosambaa katika mitandao ya kijamii, inayomuonyesha mtoto yatima aliyeiba parachichi kwa ajili ya kula na ndugu zake, akipigwa hadi kufa, mkoani Iringa. Anaripoti Zakia Nanga, Dar es Salaam … (endelea).
Uchunguzi wa haraka na wa kina kuhusu picha hiyo tayari umeanza mara moja.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa ndiye anayeongoza msako na ufuatiliaji wa tukio hilo. Jeshi la Polisi limesema taarifa kamili zitatolewa mara uchunguzi utakapokamilika.
Aidha, Polisi wamewashukuru wananchi wote wanaoendelea kushirikiana kwa kutoa taarifa muhimu zinazosaidia katika ufuatiliaji wa tukio hilo. Ushirikiano huo umetajwa kuwa chachu katika kufanikisha uchunguzi.
ZINAZOFANANA
Madaktari sita wanusurika kifo Mwanza
‘Camp’ ya macho CCBRT Mbagala yavuta mamia ya wakazi wenye matatizo
Wazili Mkuu kuongoza mazishi ya Kitaifa ya Lukuvi Idodi Iringa