
RAIS wa zamani wa Zambia Edgar Lungu amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 68, chama chake kimesema. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
“Amekuwa akipokea matibabu maalum nchini Afrika Kusini” kwa ugonjwa ambao haujatajwa, chama cha Patriotic Front kilisema kikithibitisha habari hiyo.
Lungu aliongoza Zambia kwa miaka sita kuanzia 2015, na kushindwa katika uchaguzi na Rais wa sasa Hakainde Hichilema kwa kura nyingi.
Baada ya kushindwa katika uchaguzi huo alijiondoa kwenye siasa lakini baadaye akarejea na kuonekana kuwa na nia ya kugombea tena urais
ZINAZOFANANA
Tanzania yang’ara wakaguzi wa majitaka migodini kimataifa
Thabo Mbeki atua Tanzania kushiriki maadhimisho ya Siku ya Afrika
Kadinali Robert Prevost atangazwa kuwa Papa mpya