September 18, 2024

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Ukraine yatangaza kupungukiwa silaha

Volodymyr Zelensky

 

RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, amesema kwamba taifa hilo halina silaha zinazoweza kuwatosheleza wanajeshi wake. Kyiv, Ukraine.

Akizungumza jana Jumapili, Rais Zelensky alisema kwamba Ukraine inahitaji kuzipatia silaha brigedi 14, lakini uwezo wake ni brigedi 4 pekee.

Zelensky alimwambia mwandishi wa habari wa Marekani, Fareed Zacharia kwenye mahoajiano ambayo pia yalichapishwa kwenye mtandao wa Telegram na vyombo vya habari vya Ukraine.

Zelensky amesema Ukraine imetumia akiba yake yote na hasa wakati Bunge la Marekani lilipozuia upelekwaji wa silaha na kusisitiza kwamba ni lazima hifadhi yake iwe na silaha tena.

About The Author