September 16, 2024

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Hospitali Sinza, Meridianbet kuimarisha Afya ya wagonjwa

 

Usalama na Afya ni jambo la msingi sana, na kila mtu anapambana kwa gharama kubwa kuhakikisha afya yake inakuwa imara, juhudi hizo pekee hazitoshi kwa serikali peke yake kuhakikisha suala la afya kwa nchi nzima linakuwa imara, bali linategemea wadau kama Meridianbet na wengine kuongeza nguvu kwenye masuala ya Afya.

Kampuni namba moja ya michezo ya ubashiri na kasino ya mtandaoni, Meridianbet imepongezwa na Hospitali ya Sinza, kwa juhudi zao za kuhakikisha jamii inapata huduma bora za afya.

Hii ni baada ya kutoa msaada wa vyandarua salama katika Hospitali hiyo, inayotoa huduma mbalimbali kwa wakazi wa Sinza na watanzania wote.

Katibu wa Hospitali ya Sinza Fadhili Kavishe akipokea msaada huo alisema kuwa utaenda kusaidia huduma za IPD- za kulaza wagonjwa.

“Kwa niaba ya uongozi wa Hospitali ya Sinza, natoa shukrani kwa Meridianbet kwa msaada huu, kama hospitali tumekuwa na mahitaji makubwa kwa kipindi cha nyuma na sasa, tukizingatia Hospitali hivi karibuni imezindua huduma za kulaza wagonjwa (IPD).

“Kwa kiasi kikubwa kuna mahitaji makubwa ya neti kwaajili ya kulaza wagonjwa huku tukiamini kwamba, tuna changamoto kubwa ya ugonjwa wa Malaria katika nchi yetu, kwahiyo kwa kiasi kikubwa utasaidia kukinga wagonjwa wetu wasiweze kupata ugonjwa huo” Alisema Fadhili Kavishe.

Meridianbet wakali wa michezo ya kasino ya mtandaoni inaendeleza utamaduni wake wa kurudisha kwa jamii, na kuifanya yenye tabasamu muda wote, hii ni kwa mujibu wa Nancy Ingram muwakilishi wa kampuni hiyo.

“Tunafahamu ugonjwa wa Malaria ni changamoto kubwa nchini, katika kuhakikisha usalama wa wagonjwa mahospitalini dhidi ya ugonjwa huo, tumeweza kutoa vyandarua mahususi kwa wagonjwa.”

NB: Meridianbet wanakupa nafasi ya kuendelea kubashiri na kushinda kila unapojisajili, ili kubeti na kucheza kasino ya mtandaoni unapaswa kujisajili na kisha unapewa bonasi ya ukaribisho. Jisajili hapa.

About The Author