
MABIGWA wa soka nchini, Young Africans, wanaanza safari yao ya kutetea ubingwa hivi leo 24 Septemba 2025, kwa kukutana TP Lindanda (Pamba Jiji Fc), katika dimba la Benjamin Mkapa, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Mchezo huo, unaotarajiwa kuanza majira ya saa 1:00 usiku, ni muendelezo wa michezo ya Ligi Kuu ya soka ya NBC, ambapo leo kutakuwa mechi mbili.
Mbali na mechi kati ya Yanga na Pamba Jiji, mchezo mwingine unawakutanisha Azam Fc (Wanalambalamba) dhidi ya Mbeya City FC almaarufu Purple Nation. Mchezo huo, utapigwa katika dimba la Azam Complex, Chamazi majira ya saa 3:00 usiku
ZINAZOFANANA
Jiji la Dodoma kupata uwanja mpya wa kisasa wa michezo
Uwanja wa Mkapa wakarabatiwa kwa Sh. 31 bilioni
Europa League kukupeleka moja kwa moja kwenye ushindi wa Meridianbet.