Jair Bolsonaro
MAHAKAMA nchini Brazil imemhukumu kifungo cha miaka 27 na miezi mitatu jela aliyekuwa Rais wa Taifa hilo, Jair Bolsonaro, baada ya kumkuta na hatia ya kupanga njama za kupindua Serikali. Inaripoti Mitandao ya Kijamii … (endelea).
Uamuzi uliopitishwa na Majaji wanne kati ya watano waliosikiliza Kesi, umeonesha baada ya kushindwa katika Uchaguzi, Bolsonaro aliandaa mikakati ya kumuua mpinzani wake, Rais Luiz Inácio Lula da Silva.
Mawakili wa kiongozi huyo wamewasilisha Rufaa kupinga kesi hiyo pamoja na kutaka awekwe chini ya ulinzi akiwa nyumbani kwake badala ya kupelekwa Gerezani.
ZINAZOFANANA
Tume.yamtangaza Museven mshindi Urais Uganda
Watu 100 wameuawawa shambulio la kukamatwa Maduro
Kiongozi wa kijeshi Burkina Faso anusuruka kuuawa