
Kardinali Giovani Angelo Becciu
KARDINALI Giovani Angelo Becciu wa Serdegna ametangaza kujitoa kushiriki kwenye mkutano wa uchaguzi wa Papa mpya unaotarajia kufanyika tarehe 7 Mei 2025. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Kardinali Giovani ametoa maamuzi hayo huku akisisitiza kutokuwa na hatia ila imempasa kutii utashi wa baba mtakatifu Francis kwa ajili ya maslahi ya kanisa.
Hatua hio ya kardinali Giovani imetokea wakati kanisa katoliki likijiandaa kwa mkutano wa kumchagua Papa mpya baada ya kifo cha papa Francis na nafasi kubaki wazi.
Baada ya kifo cha papa francis kanisa katoliki lipo kwenye maandalizi ya mchakato maalumu wa uchaguzi utakaofanyika katika kanisa la Sistine Vatican.
Kardinali Giovani amewahi kuwa mmoja wa watu wenye ushawishi mkubwa ndani ya Vatican akihudumu nafasi mbalimbali ikiwemo Naibu wa masuala ya ndani ya Vatican, na aliteuliwa na papa Francis.
Hata hivyo aliingia hatiani mwaka 2020 baada ya kuhusishwa na kashfa ya matumizi mabaya ya fedha za kanisa na zinginezo zilizopelekea Papa Francis kumwondoa katika wadhifa wake na kumpokonya haki ya kushiriki katika mikutano ya uchaguzi.
ZINAZOFANANA
Amnesty yakosoa hatua za Trump akitimiza siku 100 madarakani
Mume wa Marehemu mwimbaji wa Injili ahukumiwa kunyongwa
Matumizi ya kijeshi yaongezeka duniani kwa kiwango kikubwa