
NAIBU Rais wa Kenya Rigathi Gachagua ambaye anakabiliwa na tuhuma mbalimbali, ikiwemo ukosefu wa nidhamu na kumhujumu mkuu wake Rais William Ruto amekimbília mahakani
Vyombo vya habari nchini Kenya vimeripoti kwamba Gachagua siku ya amewasilisha ombi katika mahakama mjini Nairobi akitaka kusitishwa mchakato wa kumuondoa katika nafasi yake ulioanzishwa dhidi yake na wabunge mapema wiki hii.
Washirika wa Rais Ruto waliwasilisha maombi ya kuondolewa kwa Gachagua siku ya Jumanne wakimshtumu kuchochea chuki za kikabila na kudhoofisha serikali.
ZINAZOFANANA
Kadinali Robert Prevost atangazwa kuwa Papa mpya
Bunge la Ulaya laitaka Tanzania kumuachia huru Lissu
Waziri Mkuu wa Romania ajiuzulu