September 21, 2024

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Kaa mkao wa kula na Meridianbet Jumamosi ya leo

 

Wikendi ya kutusua na Meridianbet hatimaye imefika sasa, unangoja nini suka jamvi lako kuaniza kule  Uingereza, Hispania, Italia na kwingine kwingi utimize ndoto zako hapa.

Ligi pendwa Duniani EPL leo kuna mechi kibao za pesa Aston Villa baada ya kushinda mechi yake iliyopita, leo atamualika Wolves ambaye hajashinda mechi yoyote hadi sasa. Unai Emery na vijana wake wanahitaji kuendelea kufanya vizuri huku Mbwa Mwitu wakitaka angalau leo washinde. Je wataweza mbele ya Villa yenye ubora?. Mechi hii ina ODDS 1.54 kwa 5.48. Bashiri sasa.

Baada ya kupoteza mechi iliyopita akiwa nyumbani, leo tena Liverpool atakuwa Anfield kukiwasha dhidi ya AFC Bournemouth ambaye alipoteza pia mechi yake akiwa nyumbani. Arne Slot na vijana wake wanauhitaji mchezo huu wa leo kwa hali na mali kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kuwania ubingwa.

Meridianbet wanampa nafasi ya ushindi Liver kwa ODDS 1.28 kwa 8.62 huku mara ya mwisho kukutana Jogoo aliondoka na ushindi mnono. Je mgeni anaweza kulipa kisasi leo ugenini?. Jisajili hapa.

Meridianbet inakupa nafasi ya kuondoka na mshiko wako leo ukibashiri mechi za Ijumaa ya leo. Pia cheza michezo ya Kasino ya mtandaoni kama vile, Poker, Super Heli, Roullette, Aviator, Wild Icy Fruits, Keno na mingine kibao.

Naye Newcastle United atakuwa ugenini kukiwasha dhidi ya Fulham ya Marco Silva majira ya saa 11:00 jioni. Tofauti ya pointi kati yao ni 5 huku mtanange wa mwisho kukutana, Eddie Howe na vijana wake walishinda. Mwenyeji atakubali kuendelea kuwa mteja wa Newcastle?. Beti mechi hii yenye ODDS 2.69 kwa 2.50.

Saa 1:30 usiku Manchester United atakuwa mgeni wa Crystal Palace ambaye hajashinda mechi yoyote kati ya 4 alizocheza. Man U chini ya Ten Hag wameshinda mechi mbili pekee, na mechi ya mwisho kukutana Mashetani Wekundu walipoteza kwa kipigo kizito. Je leo watafanya nini ugenini? 2.79 kwa 2.35 ndio ODDS za mechi hii. Bashiri sasa.

Vilevile unaweza kupiga maokoto na ligi kuu ya Hispania LALIGA, CA Osasuna atamualika UD Las Palmas ambaye anashika nafasi ya 19 kwenye ligi akiwa na pointi 2 pekee. Mwenyeji yupo nafasi 13 akiwa na pointi 7. Meridianbet wameipa mechi hii ODDS 1.91 kwa 4.11 Jisajili sasa.

Valencia CF ambaye anashika mkia atakuwa mwenyeji wa Girona ambaye yupo nafasi ya 7. Mwenyeji kwenye mechi 5 ambazo kacheza amepoteza 4 na kutoa sare moja wakati mgeni yeye kashinda mbili, sare moja, na kupoteza mbili. Je kwa ODDS 2.65 kwa 2.69 nani kuondoka na pointi 3?. Tengeneza jamvi hapa.

Bingwa mtetezi, Real Madrid atapepetana dhidi ya Espanyol Barcelona majira ya saa 4:00 usiku. Ancellotti na vijana wake wanapendelewa kuchukua ushindi leo kwa ODDS 1.15 kwa 16.66. Beti yako unaiweka wapi hapa?

Ligi kuu ya Italia SERIE A, pia inaendelea  Venezia mabao wamepanda daraja msimu wataumana dhidi ya Genoa. Mwenyeji mpaka sasa kwenye mechi 4 alizocheza ameambulia pointi moja pekee huku mgeni wake akikusanya pointi 5 pekee. Suka jamvi mechi hii yenye machaguo zaidi ya 1000 Meridianbet.

Na mechi kali leo ni hii ya Juventus dhidi ya Napoli ya Antonio Conte majira ya saa 1:00 usiku. Tofauti ya pointi kati yao ni moja pekee. Timu hizi zote zina makocha wapya lakini mara ya mwisho walipoonana Napoli walishinda. 2.25 kwa 3.28 ndio ODDS za mechi hii. Suka mkeka wako sasa.

BUNDESLIGA ni kivumbi leo Union Berlin atakiwasha dhidi ya TSG Hoffenheim huku timu hizi zote zikiwa zimeshinda mechi moja moja tuu kati ya 3. Meridianbet wanampa mwenyeji nafasi kubwa kushinda leo kwa ODDS 1.87 na 3.82. Wewe unampa nani?. Jisajili hapa.

FC Heidenheim atakuwa uso kwa uso dhidi ya SC Freiburg ambapo timu zote zina pointi 6 mpaka sasa. Kutokana na ukali wa mechi hii, Meridianbet wameipatia ODDS 2.79 kwa 2.43. Bashiri hapa sasa.

Bayern Munich atakuwa ugenini dhidi ya Werder Bremen. Bayern anaingia dimbani akikumbuka kichapo cha bao moja alichopokea mechi ya mwisho walipokuta akiwa kwake. Timu hiyo ambayo kwasasa inanolewa na Vincent Kompany wanataka ushindi leo kwa hali yoyote. Je wataweza?. Mechi hii ina machaguo zaidi ya 1000. Beti kijanja.

Unaweza ukajibweda na ODDS KUBWA pia kwenye ligi kuu ya Ufaransa LIGUE 1, Lille atakuwa mwenyeji wa Strasbourg huku tofauti ya pointi kati yao ikiwa ni moja pekee. Mechi ya mwisho kukutana Lille alishinda. Je nani leo ataibuka na ushindi?. Bashiri hapa.

Pia Stade Rennes baada ya kushinda mechi yake iliyopita, leo atakuwa nyumbani kutunisha misuli dhidi ya RC Lens ambaye alitoa sare ya bila kufungana mechi yake iliyopita. Mechi mbili za msimu uliopita zote walizokutana walitoa sare. Je msimu huu nani kuibuka mbabe? Mechi hii imepewa ODDS 2.40 kwa 2.94. Suka mkeka hapa.

Bingwa mtetezi wa Ufaransa PSG atakuwa mgeni wa Reims mchezo ambao utapigwa majira ya saa 4:00 usiku. Meridianbet wamempa Paris nafasi ya kushinda kwa ODDS 1.44 kwa 6.27. Mara ya mwisho kukutana, walitoa sare. Jisajili hapa.

About The Author