RAIS wa Marekani, Donald Trump amesema nchi yake inaweza kuanzisha mfumo wa kutoza ada kwa meli zinazopita katika Mlango wa Hormuz baada ya vita kumalizika, akidai kuwa Marekani ndiyo mshindi wa mapambano hayo. Anaripoti mwandishi wetu, Dar es Salaam …(endelea).
Kauli hiyo imekuja wakati mvutano ukiendelea Mashariki ya Kati, ambapo njia hiyo muhimu ya usafirishaji wa mafuta duniani imeathiriwa na vita vinavyoendelea.
Akizungumza na waandishi wa habari, Trump amependekeza kuwa badala ya Iran kutoza ada kwa meli, Marekani inaweza kufanya hivyo yenyewe, akisisitiza kuwa ina haki hiyo kutokana na ushindi wa kijeshi.
“Kwa nini sisi tusitoze? Sisi ndio washindi,” amenukuliwa Trump.
Mlango wa Hormuz ni njia muhimu inayounganisha Ghuba ya Uajemi na Bahari ya Hindi, na hupitisha takribani asilimia 20 ya mafuta ya dunia.
ZINAZOFANANA
Gavana wa zamani Urusi ahukumiwa miaka 14 Gerezani kwa Rushwa
Milio ya risasi yasikika karibu na Ikulu ya Marekani, uchunguzi waanza
Rais Tshisekedi awatunuku nyumba na gari kila mchezaji kwa kufuzu kombe la Dunia