April 7, 2026

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Trump atoa tishio jipya kwa Iran

Spread the love

RAIS wa Marekani Donald Trump ametoa tishio jipya kwa Iran akionya kwamba mashambulizi makubwa yanaweza kutokea leo usiku huku muda wa mwisho aliotoa kwa Iran kufanya makubaliano na kufungua Mlango-Bahari wa Hormuz ukikaribia. Anaripoti mwandishi wetu, Dar es Salaam …(endelea).

Trump amechapisha kwenye mtandao wa Truth akionya mfumo mzima utaangamizwa leo na hautarejeshwa tena.

“Tutabaini usiku wa leo,moja ya nyakati muhimu zaidi katika historia ndefu na ngumu ya dunia,miaka 47 ya dhuluma,ufisadi na vifo hatimaye itafikia mwisho.Mungu awabariki watu wa Iran”Alisema Donald Trump

Tishio hilo linakuja siku moja baada ya Trump kusema kwamba Marekani itaharibu kila daraja na kituo cha nishati nchini Iran ikiwa makubaliano hayatafikiwa .

About The Author

error: Content is protected !!