April 8, 2026

Mwanahalisi Online

Habari za Uhakika

Rais Tshisekedi awatunuku nyumba na gari kila mchezaji kwa kufuzu kombe la Dunia

Spread the love

 

RAIS Félix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) amemtunuku kila Mchezaji wa timu ya Taifa ya soka gari na nyumba baada ya kufuzu kwa kombe la Dunia mwaka huu kwa kuifunga Jamaica bao 1-0.Anaripoti mwandishi wetu, Dar es Salaam …(endelea).

Picha zilizotolewa na Ofisi ya Rais wa DRC zinamuonyesha Rais Tshisekedi akiwakaribisha Wachezaji wa timu ya Taifa ya Les Léopards jana katika Mji Mkuu Kinshasa, walipowasili nchini humo.

Taarifa hiyo ilisema kuwa katika kuwashukuru timu hiyo, alimpa kila Mchezaji Nyumba na gari, kwa kuirejesha DRC kwenye michuano ya Kombe la Dunia baada ya kushiriki mara ya mwisho mwaka 1974.

DRC iko Kundi K pamoja na Ureno, Uzbekistan na Colombia.

Itacheza mechi yake ya kwanza dhidi ya Ureno 17 Juni mwaka huu, kwenye michuano ya Kombe la Dunia itakayofanyika

About The Author

error: Content is protected !!