MCHEZAJI nyota wa Ligi Kuu ya Uingereza, Kurt Zouma anaweza kufunguliwa mashtaka baada ya kurekodiwa kwenye video akimpiga paka wake kama mpira kwenye sakafu ya jikoni yake.
Nyota huyo wa West Ham (27), pia ameonekana akimpiga kofi usoni paka huyo.
Klabu hiyo imelaani kitendo chake na kusema itashughulikia suala hilo ndani.
Beki huyo wa West Ham anaonekana akimshambulia mnyama huyo kwenye jumba lake la kifahari la pauni milioni 2 huku kaka yake akichukua video.
Zouma ameonekana akimdondosha paka huyo na kisha kumpiga teke hewani kwenye sakafu ya jikoni.
Zouma raia wa Ufaransa pia ameonekana akimfukuza mnyama huyo kuzunguka chumba chake cha kulia chakula mbele ya mtoto huku mpigapicha akicheka.
Katika clip ya mwisho, anaonekana akimpiga paka kwa nguvu usoni – na kutoka kwa mikono ya mtoto.
Jana usiku tarehe 8 Februari, 2022, Zouma ameomba radhi kwa shambulio hilo na kusisitiza kuwa lilikuwa tukio la pekee.
Amesema; “Naomba msamaha kwa vitendo vyangu. Hakuna visingizio kwa tabia yangu, ambayo ninajutia kwa dhati.”
Leave a comment