Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Zogo bungeni, wapinzani wafura
Habari za Siasa

Zogo bungeni, wapinzani wafura

Bunge la Tanzania
Spread the love

HATUA ya Bunge la Jamhuri kupitisha Mswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria mbalimbali (Na.5) wa mwaka 2019, imetibua wapinzani. Anaripoti Danson Kaijage
 … (endelea).

Muswada huo umepitishwa huku malalamiko kutoka upinzani yakitawala.

Upinzani imepinga kwa madai, kolamu ya wabunge haikutimia kwa mujibu wa kanuni za Bunge.

Nagima Giba, Mwenyekiti wa Bunge ndiye aliongoza kikao cha bunge wakati wa kuchangia na kupitisha muswada huo leo tarehe 6 Septemba 2019.

Baada ya wabunge kumaliza kuchangia na kutaka bunge likae kama kamati kwa ajili ya kupitisha vifungu, wabunge wa upinzania walidai kuwa akidi haikuwa imetimia.

Ester Bulaya ambaye ni Mbunge wa Bunda, aliomba utaratibu ili kueleza bunge kutokidhi kwa akidi, lakini Giga alimnyima nafasi hiyo.

Wabunge hao walipaza sauti kusisitiza juu ya kutokidhi kwa akidi katika kupitisha miswada huo. Giga aliwapuuza.

Wabunge walisisitiza kuwa wamefanya hesabu na kubaini wabunge waliopo ni 63, hivyo akidi ya wabunge haikuwa imekamilika na kwamba wanavunja kanuni.

Hata hivyo Giga alisema, zipo kamati tatu zote zinafanya kazi na zimejiridhisha kuwa akidi imekamilika.

Hali hiyo ilisababisha zogo kutokana na wapinzani kutoridhika na uamuzi wa Giga.

Hata hivyo, Giga aliwataka wapinzania wanapokuwa wakifanya marekebisho ya sheria, wapate msaada kutoka kwa wanasheria ili kufanya marekebisho kukubalika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!