Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa ZLSC yaipeleka ZEC kortini Z’bar
Habari za Siasa

ZLSC yaipeleka ZEC kortini Z’bar

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar (ZLSC), kimefungua kesi ya Kikatiba katika Mahakama Kuu ya Zanzibar, kupinga Sheria ya Uchaguzi. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo tarehe 10 Oktoba 2019 na Ofisi ya Mawasiliano ya ZLSC, inaeleza kwamba kesi hiyo imefunguliwa Oktoba Mosi mwaka huu na kupewa namba 3/2019.

Taarifa hiyo inaeleza kuwa, kesi hiyo imefunguliwa ili Mahakama Kuu ya Zanzibar itoe ufafanuzi juu ya uhalali wa kuwepo kwa kifungu cha 143 cha Sheria ya Uchaguzi Nambari 4 ya mwaka 2018, ambacho kinazungumzia uwezo na mamlaka ya jumla ya Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC).

Kituo hicho kinadai kuwa, kifungu hicho kinaeleza tume itakua na uwezo, jukumu na mamlaka katika kuamua jambo lolote linalohusiana na uchaguzi, ambalo halikuwekewa masharti katika sheria na uamuzi wake utakuwa wa mwisho na hautahojiwa na mamlaka yoyote.

“Kituo kimeamua kufungua Shauri la Kikatiba katika Mahakama Kuu ya Zanzibar. lengo na madhumuni ya ZLSC ni kutafuta ufafanuzi wa Mahakama Kuu juu ya uhalali wa kuwepo kwa kifungu hicho,” inaeleza taarifa hiyo na kuongeza ;

“Hivyo kituo kimeona kwamba, iko haja ya kupata ufafanuzi na tafsiri ya kifungu hicho cha 143 katika Mahakama Kuu ya Zanzibar ambayo ni mahakama ya kumbukumbu kama ilivyoelezwa katika kifungu cha 93 (1) cha Katiba ya Zanzibar (1984).”

ZLSC kimeeleza kwamba, kwa mara ya kwanza kesi hiti imetajwa mahakamani hapo, leo tarehe 1 Oktoba 2019

“Kituo kinafanya hivyo ili kuhakikisha sheria haziendi kinyume na katiba sambamba na kuzingatia misingi ya demokrasia na haki za binadamu,” inaeleza taarifa ya kituo hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!