Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto, Lissu wamkosha Maalim Seif
Habari za SiasaTangulizi

Zitto, Lissu wamkosha Maalim Seif

Tundu Lissu akiwa Zitto Kabwe
Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, Mshauri Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo anatarajia mwelekeo mpya wa vyama vya upinzani nchini baada ya Zitto Kabwe na Tundu Lissu kukutana na kuzungumzia namna ya ushirikiano. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Zitto ambaye ni Kiongozi Mkuu wa ACT-Wazalendo, alikwenda kumjulia hali Lissu nchini Ubelgiji anakopatiwa matibabu baada ya kushambuliwa kwa risasi jijini Dodoma ‘Area D’ tarehe 7 Septemba 2019.

Lissu ambaye ni Mwanasheria Mkuu wa Chadema na aliyekuwa mbunge wa jimbo la Singida Mashariki, alikutana na Zitto na kufanya mazungumzo yanayolenga namna ya kushirikiana kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter tarehe 3 Septemba 2019, Maalim Seif ameandika kuwa Zitto na Lissu wameleta faraja kwa wadau wa siasa hasa za upinzani kwa kuonesha njia kuelekea 2020.

Maalim Seif amewapongeza wanasiasa hao kwa hatua hiyo, na kuwataka wazidi kushirikiana kwa pamoja katika kubadilisha historia ya Tanzania kupitia uchaguzi wa 2020.

Mwanasiasa huyo mkongwe hapa nchini, ameeleza  kwamba uchaguzi huo nimuhimu kuliko chaguzi zote katika kuamua mustakabali wa Tanzania.

Ameandika “Zitto Kabwe na Tundu Lissu wametupa faraja na kutuonesha njia kuelekea 2020. Nawapongeza na kuwatia moyo kutekeleza wajibu wa kihistoria kwa Tanzania wakati tunaelekea uchaguzi mkuu wa 2020 ambao ni uchaguzi muhimu kuliko chaguzi zote katika kuamua mustakbali wa Tanzania.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

error: Content is protected !!