MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi, Abdulrahman Kinana, anatarajiwa kupokea kijiti cha uongozi wa kituo cha demokrasia Tanzania (TCD). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Taarifa hiyo imetolewa leo Jumanne tarehe 5 Aprili 2022 na Mwenyekiti wa sasa wa TCD, Zitto Kabwe, wakati wa hotuba yake kwenye mkutano wa kitaifa wa maridhiano, haki na amani ulioandaliwa na kituo hicho.
Zitto ambaye pia ni Kiongozi wa ACT-Wazalendo amesema atakabidhi uongozi huo kwa chama cha mapinduzi kesho Jumatano tarehe 6 Aprili 2022, baada ya muda wake kumalizika tangu Februari mwaka huu.
Amesema aliendelea kuongoza TCD hadi sasa kutokana na kuahirishwa mara kwa mara kwa mkutano wake hivyo wajumbe wengine wakamtaka kukamilisha kwanza mkutano huo kabla ya kuondoka.
TCD ni taasisi isiyo ya kiserikali inaundwa na vyama vya siasa nchini vyenye uwakilishi bungeni, baraza la wawakili na kwenye mabaraza ya madiwani.
Vyama vinavyounda TCD kwa sasa ni pamoja na CCM, ACT-Wazalendo, Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na NCCR-Mageuzi.
Leave a comment