Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto kufuata nyayo za Tundu Lissu
Habari za SiasaTangulizi

Zitto kufuata nyayo za Tundu Lissu

Zitto Kabwe na Tundu Lissu
Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amefuata nyayo za Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, kufanya ziara nchini Ujerumani. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea). 

Zitto ambaye yuko nchini Ujerumani, leo tarehe 21 Februari 2019 atafanya mazungumzo na asasi za kiraia mjini Berlin nchini Ujerumani, kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea Afrika hususan Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na John Mbozu, Katibu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ACT, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini, atahudhuria Mkutano Mkuu wa chama cha Die Linke utakaoanza tarehe 22 hadi 24 Februari 2019 mjini Bonn, Ujerumani.

“Kabla ya Mkutano huo, Ndugu Zitto atafanya mazungumzo na asasi za kiraia leo mjini Berlin, kujadiliana kuhusu masuala mbalimbali yanayoendelea Afrika hususani Tanzania,” inaeleza sehemu ya taarifa ya Mbozu.

Aidha, Zitto anatarajia kufanya mazungumzo na Rais wa European Left, Gregor Gysi. Baada ya  hapo atakutana na Mbunge wa Die Linke katika Bunge la Ujerumani, Eva Maria Schreiber ambaye ni mjumbe mwenza katika programu ya “Mbunge amlinde Mbunge”.

Katika ziara hiyo, Zitto ameambatana na Mbozu, Katibu wa Ngome ya wanawake ACT, Mwanaisha Mndeme.

Kabla ya Zitto kufanya ziara hiyo, hivi karibuni Lissu alifanya ziara nchini humo kwa muda wa siku mbili na kuzungumza na baadhi ya maofisa wa serikali na wabunge wa Bunge ka Ujerumani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!