MBUNGE wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe amewasilisha swali la maandishi bungeni akiitaka serikali iueleze umma kuhusu idadi ya kesi zilizofunguliwa kwenye mahakama za kimataifa dhidi yake. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).
Zitto ameandika hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter, ambapo ameandika kuwa swali hilo la maandishi ameliwasilisha bungeni leo tarehe 4 Septemba 2018.
“Muda mfupi uliopita nimewasilisha swali la maandishi Bungeni kuitaka Serikali iueleze umma Kuhusu kesi zote ambazo Jamhuri ya Muungano imefunguliwa kwenye mahakama za kimataifa za usuluhishi ya migogoro ya Biashara, uwekezaji na mikataba. Watanzania wanafichwa Mambo mengi muhimu,” ameandika Zitto katika ukurasa wake wa Twitter.
Muda mfupi uliopita nimewasilisha swali la maandishi Bungeni kuitaka Serikali iueleze umma Kuhusu kesi zote ambazo Jamhuri ya Muungano imefunguliwa kwenye mahakama za kimataifa za usuluhishi ya migogoro ya Biashara, uwekezaji na mikataba. Watanzania wanafichwa Mambo mengi muhimu
— Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) September 4, 2018
Zitto ameandika kuwa, amechukua uamuzi huo baada ya kupitia nyaraka za kesi ya Acacia Mining dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kugundua kuwa kuna taarifa zinazofichwa kwa umma.
“Nimechukua uamuzi huu baada ya kupitia nyaraka nyeti za kesi ya Acacia Mining dhidi ya Jamhuri ya Muungano ( LCIA Arbitration No. UN173686 no. 87 ) iliyopo London na kugundua kuwa Serikali yetu inaficha Taarifa Kwa umma wakati Watanzania Ndio watalipa matrilioni ya shilingi,” ameandika Zitto.
Nimechukua uamuzi huu baada ya kupitia nyaraka nyeti za kesi ya Acacia Mining dhidi ya Jamhuri ya Muungano ( LCIA Arbitration No. UN173686 no. 87 ) iliyopo London na kugundua kuwa Serikali yetu inaficha Taarifa Kwa umma wakati Watanzania Ndio watalipa matrilioni ya shilingi….
— Zitto MwamiRuyagwa Kabwe (@zittokabwe) September 4, 2018
Zitto ameendelea kuandika kuwa: “Kesi iliyoamuliwa juzi dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) ilizungumzwa kwenye Taarifa ya CAG ya mwaka huu kwa Hesabu za 2016/17. Lakini pia kesi hii haikuwa yetu kwani Benki ya SCBHK haijawahi kuwa na mkataba na nchi yetu. Uzembe mkubwa umefanyika na hivyo kubambikwa kesi si yetu.”
Leave a comment