Thursday , 23 March 2023
Home Gazeti Habari Zitto: Buhigwe msitishwe
HabariHabari za SiasaTangulizi

Zitto: Buhigwe msitishwe

Zitto Kabwe kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, amewataka wakazi wa Jimbo la Buhigwe, Kigoma wasitishike na watu wanaowashinikiza kuchagua mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika jimbo hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma…(endelea).

Amesema, kumekuwepo na baadhi ya watu, baada ya kuona upepo wa kisiasa unabadilika, wameanza kuwatisha wananchi kuwa wasichague upinzani kwa kuwa, hawataleta maendeleo.

Zitto ametoa kauli hiyo jana tarehe 9 Mei 2021, katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo wakati akimnadi mgombea wake Garula Kudra.

 “Kuna watu wanaowatisha na kuwalazimisha kutowapigia kura viongozi wa vyama vya upinzani, natambua hilo eti kwa madai hawezi kuleta maendeleo.

“Nataka niwambie, maendeleo hayaletwi na chama bali viongozi bora.

Mtu bora anaweza kupatikana kwenye chama hata kama ni kidogo,” amesema Zitto.

 Uchaguzi kwenye jimbo hilo, unatarajiwa kufanyika tarehe 16 Mei 2021, ni baada ya Dk Philip Mpango, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

1 Comment

  • Asante ndugu zitto bado hujajitambua kama wakati umeshakupita kusema ni maneno matupu unachokifanya wananchi wa buhigwe hawakioni

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

error: Content is protected !!