Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Zitto: Buhigwe msitishwe
HabariHabari za SiasaTangulizi

Zitto: Buhigwe msitishwe

Zitto Kabwe kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, amewataka wakazi wa Jimbo la Buhigwe, Kigoma wasitishike na watu wanaowashinikiza kuchagua mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika jimbo hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kigoma…(endelea).

Amesema, kumekuwepo na baadhi ya watu, baada ya kuona upepo wa kisiasa unabadilika, wameanza kuwatisha wananchi kuwa wasichague upinzani kwa kuwa, hawataleta maendeleo.

Zitto ametoa kauli hiyo jana tarehe 9 Mei 2021, katika kampeni za uchaguzi mdogo wa jimbo hilo wakati akimnadi mgombea wake Garula Kudra.

 “Kuna watu wanaowatisha na kuwalazimisha kutowapigia kura viongozi wa vyama vya upinzani, natambua hilo eti kwa madai hawezi kuleta maendeleo.

“Nataka niwambie, maendeleo hayaletwi na chama bali viongozi bora.

Mtu bora anaweza kupatikana kwenye chama hata kama ni kidogo,” amesema Zitto.

 Uchaguzi kwenye jimbo hilo, unatarajiwa kufanyika tarehe 16 Mei 2021, ni baada ya Dk Philip Mpango, aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.

1 Comment

  • Asante ndugu zitto bado hujajitambua kama wakati umeshakupita kusema ni maneno matupu unachokifanya wananchi wa buhigwe hawakioni

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!