Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto amharibia JPM Kigoma
Habari za Siasa

Zitto amharibia JPM Kigoma

Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo akizungumza na wananchi wa Kigoma
Spread the love

ZITTO Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, amemchomea utambi Rais John Magufuli kwamba, amewatupa watu wa Kigoma. Anaripoti Faki Sosi, Kigoma … (endelea).

Amesema, Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imehamisha fedha za mradi wa umeme wa Malagarasi na kuzipeleka katika mradi wa umeme Stigler Gorge, Rufiji mkoani Pwani.

Amesisitiza, kwamba endapo wananchi wa Kigoma watathubutu kuichagua CCM, watakuwa wamechagua kuendelea kutengwa.

Zitto ametoa kauli hiyo mkoani Kigoma akiwa kwenye ziara yake ya Mikoa ya Magharibi, aliyoianza mwanzoni mwa wiki hii.

“Nyinyi mnafahamu, tulikuwa na mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa maji hapa Kigoma. Mradi wa umeme wa Malagarasi wa Megawati 43.

“Ukisoma Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi mwaka 2015, wameahidi ifikapo 2020 mradi wa umeme wa maji wa Malagarasi utakuwa umekamilika,” amesema Zitto.

Amesema, akiwa bungeni alimuuliza Dk. Medard Kalemani, Waziri wa Nishati kuhusu mradi huo, majibu yake yalikuwa fedha hizo zimeelekezwa katika mradi wa Stigler Gorge.

“Mwaka 2020, mimi nimeuliza ndani ya Bunge, nimemuuliza Waziri wa Nishati, Mradi wa Umeme wa Malagarasi ambao tulikuwa tumekwishapewa fedha na Benki ya Maendeleo ya Afrika umefikia hatua gani?

“Waziri akasema, sasa hivi serikali inafanya mradi mmoja tu wa Stigler Gorge, kwa hiyo fedha za mradi wa umeme wa Malagarasi Kigoma wamepeleka knweye Stigler Gorge, sisi tumeachwa,” amesema Zitto.

Rais John Magufuli

Akisisitiza umuhimu wa mradi huo, Zitto amesema ulitarajiwa kuzalisha Megawati 43 ana kwamba, kw amatumizi ya Kigoma ambayo hayaziti Megawati 20, Kigoma ingeweza kuuza umeme Burundi.

“Sisi umeme wetu wa Malagarasi ni Megawati 43, matumizi ya Kigoma hayazidi Megawati 20, tungeweza kuwauzia hata Burundi. Watu wa Kigoma mkichagua CCM, maana yake mmekubali kuendelea kutengwa,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!