Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto afungua kesi kupinga Prof. Assad kuondolewa madarakani
Habari za Siasa

Zitto afungua kesi kupinga Prof. Assad kuondolewa madarakani

Spread the love

ZITTO  Kabwe, Kiongozi  Mkuu wa ACT wazalendo, amefungua kesi ya Kikatiba katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kupinga Uteuzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) uliofanywa na Rais John Magufuli. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kesi hiyo ya Kikatiba namba 1/2020 iliyofunguliwa na Wakili Rugemeleza Nshala, kwa niaba ya Zitto, imepangwa kusikilizwa na Majaji Mlacha, Dk. Benhajj Masoud na Masabo katika mahakama hiyo.

Zitto amefungua kesi hiyo kupinga Sheria ya Ukaguzi namba 11/2008 na pamoja na uteuzi wa CAG Charles Kichere, kwa madai kwamba, ulikuwa kinyume na masharti ya Katiba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Suphian Juma, Afisa Habari wa ACT-Wazalendo, Zitto anaiomba mahakama hiyo kubatilisha uteuzi wa CAG Kichere.

“Zitto anaiomba Mahakama kutamka kuwa,  kifungu cha 6(1) cha Sheria ya Ukaguzi namba 11 ya mwaka 2008 inaenda kinyume na Katiba. Kwa kukiuka Ibara ya 144(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na pia kupingana na kifungu 62(a) cha Sheria ya Ukaguzi, ambacho kinaendana na Katiba,” inaeleza taarifa ya Suphian na kuongeza;

“Aidha Zitto anaiomba Mahakama kutamka pia,  uamuzi wa Rais Magufuli wa kumwondoa Ofisini Prof.  Mussa Assad ulikuwa kinyume na Katiba. Kwa sababu Prof. Assad hakuwa ametimiza miaka 65 ya kisheria wala miaka 60 ya Kikatiba. Pia kwamba uteuzi wa Bwana Kichere ufutwe kwa sababu ya kukiuka Katiba.”

Kwa mujibu wa taarifa ya Suphian, Shauri hilo litaitwa kwa mara ya kwanza tarehe 28 Januari , 2020.

https://twitter.com/ACTwazalendo/status/1221043980613246976

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!