Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto aanzisha mashambulizi CCM, serikali
Habari za Siasa

Zitto aanzisha mashambulizi CCM, serikali

Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo
Spread the love

ZITTO Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini ameivaa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwamba ni katili. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwenye ukurasa wake wa Twitter Zitto ameeleza kushangazwa na ukimya wa CCM wakati wakulima wa korosho wakiteketea.

Zitto ameandika; “Serikali katili inadhulumu jasho la Wananchi masikini. Wakulima wanarejeshewa Korosho zao sasa.

“CCM hawawezi hata kupaza sauti kukemea ukatili unaofanywa na Serikali yao. Dhulma kwa mtu mnyonge ni mbaya sana.”

Serikali hivi karibuni imetangaza kufungua milango kwa wafanyabiashara wa korosho kwenda kununua zao hilo.

Katika msimu huu zao hilo limeingia mdudu baada ya kuwepo mvutano wa bei ya ununuzi ambapo serikali iliingilia katika na kununua zao hilo.

Hata hivyo, malalamiko kwa serikali kushindwa kukidhi ununuzi huo yamekuwa yakisikika.

Miongoni mwa wabunge wanaoishutumu serikali kufanya uzembe katika ununuzi wa zao hilo hivyo kutaabisha wakulima ni Nape Nnauye, Mbunge wa Mtama, Suleiman Bungara (Kilwa Kusini) na Hawa Ghasia (Mtwara Vijijini).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!