Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto: 2025 tutakuwa na uchaguzi mbaya
Habari za Siasa

Zitto: 2025 tutakuwa na uchaguzi mbaya

Spread the love

KIONGOZI wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amedai kama dosari zinazoendelea kujitokeza katika chaguzi ndogo visiwani Zanzibar, hazitatokomezwa, Uchaguzi Mkuu wa 2025 utakuwa mbaya zaidi ya Uchaguzi Mkuu wa 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar…(endelea).

Zitto ametoa kauli hiyo leo Jumatatu, visiwani Zanzibar, akibainisha dosari 15 zinazodaiwa kujitokeza katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mtambwe, uliofanyika tarehe 28 Oktoba mwaka huu, ambapo aliyekuwa mgombea wa ACT-Wazalendo, Dk. Mohamed Ali Suleiman, alitangazwa kuwa mshindi.

“Mnafahamu mambo mbalimbali yalifanyika ambayo sisi tunaona kama ishara mbaya na hasi tunapoelekea uchaguzi mkuu wa 2025. Matarajio yote ambayo tumekuwa nayo kwa ajili ya mageuzi ya kiuchaguzi hapa Zanzibar ni kama mambo hayaendi kokote,” amesema Zitto.

Zitto amesema “sababu kila jambo ambalo limelalamikiwa katika uchaguzi wa 2020, limetokea katika uchaguzi mdogo wa Mtambwe na si Mtambwe peke yake, limetokea katika chaguzi ndogo zilizofanyika hapa Zanzibar.”

Akitaja dosari hizo, Zitto alidai daftari la wapiga kura lilikuwa na wapiga kura hewa, baadhi ya wapiga kura kupewa kura zaidi ya moja, baadhi ya watendaji wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), kuingia vituoni wakiwa na kura mifukoni na kutumbukiza kwa nguvu kwenye masanduku ya kura wakati wa kuhesabu kura.

Dosari nyingine zilizotajwa na Zitto ni baadhi ya wasimamizi wa kura kuziharibu kwa makusudi hususan za wapiga kura wanaobaika ni wa ACT-Wazalendo, ili kuwa na kura nyingi zilizoharibika kumpunguzia ushindi mgombea wa chama hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

error: Content is protected !!