Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Zidane: Ramos ‘Fit’ dhidi ya Chelsea
Michezo

Zidane: Ramos ‘Fit’ dhidi ya Chelsea

Sergio Ramos, Nahodha wa Real Madrid
Spread the love

 

KOCHA wa kikosi cha Real Madrid Zinedine Zidane amethibitisha kurejea kwa naohodha wa kikosi hiko Sergio Ramos kwenye mchezo wa leo wa nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Chelsea. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa mzunguko wa pili wa nusu fainali utachezwa kwenye Uwanja wa Stamford Brigde majira ya saa 4 usiku mara baada ya kutoka sare ya bao 1-1 kwenye mchezo wa kwanza.

Ramos anarejea Uwanjani mara baada ya kukosekana kwenye mchezo uliopita kutokana na kusumbuliwa na majeruhi ya misuli ya mguu.

Kuelekea mchezo huo Zidane amesema kuwa nahodha na kiongozi wake anaerejea uwanjani kwenye mchezo wa leo na yupo tayari kucheza.

“Nahodha wetu na kiongozi amerejea na yupo na sisi, yupo tayari kucheza” alisema Zidane

Zinedine Zidane kocha wa kikosi cha Real Madrid

Nahodha huyo mwenye miaka 35 ndio mchezaji mkongwe kwenye kikosi hiko kwa sasa ambaye amebeba mataji mengi ya Ligi Kuu na klabu bingwa barani Ulaya.

Kwenye mchezo wa leo Real Madrid inahitaji ushindi wa aina yoyote au sare ya mabao kuanzia 2-2 na kuendelea ili iweze kufuzu kwenye hatua ya Fainali.

Chelsea wanaingia kwenye mchezo wa leo huku wakiwa na faida na matokeo ya mchezo wa kwanza wa bao 1-1, na hivyo kuwa na faida na bao la ugenini.

Kwenye mchezo wa leo Chelsea inahitaji ushindi wa aina yoyote ili iweze kufuzu kwenye fainali ya michuano hiyo itakayochezwa Juni 28, 2021 jijini Instabul nchini uturuki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!