Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Zahera alia na Dk. Msolla, adai amemgeuka
Michezo

Zahera alia na Dk. Msolla, adai amemgeuka

Spread the love

MWINYI Zahera, aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga, ametoa hadharani siku moja baada ya kufutwa kazi katika klabu hiyo, na kudai kuwa Mwenyekiti wa Yanga, Dk. Mshindo Msolla amemgeuka. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Zahera amesema uongozi wa Yanga umemgeuka, kwa madai kwamba walimhakikishia kuwa ataendelea kuinoa klabu hiyo, hata kama itafanya vibaya katika michuano ya kimataifa.

Zahera ameeleza kuwa, Dk. Msolla alimueleza kwamba uongozi wa klabu hiyo unamuunga mkono, licha ya kwamba mashabiki na wanachama walitaka kumng’oa.

“Mwenyekiti aliniambia, Kocha  hao sio wote mashabiki wa Yanga, sisi uongozi tuko pamoja na wewe, ” amesema Zahera.

Hata hivyo, Zahera amesema Mwenyekiti huyo alimdokeza kwamba, kuna baadhi ya viongozi wa Yanga walitaka kumng’oa, lakini harakati zao ziligonga mwamba kutokana na hoja zao kukosa mashiko.

Zahera amesema: “Mwenyekiti (Dk. Msolla) alinimbia kuwa aliambiwa na Ndama kwanini wasinifukuze, lakini Mwenyekiti akamwambia atoe sababu za kuniondoa. Alimwambia kufungwa na Pyramids ni ajabu kubwa? Hakuna mtu atashangaa, akamjibu sisi tumuonde kocha kwa sababu gani?”

Kocha huto Mkongo ameeleza kuwa, Mwenyekiti alimshauri kuwahimiza wachezaji kujituma uwanjani, kwani timu ikifanya vizuri wanachama na mashabiki hawatasema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

error: Content is protected !!