Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yazindua mfumo wa mabadiliko
Michezo

Yanga yazindua mfumo wa mabadiliko

Jengo la Yanga
Spread the love

MWENYEKITI wa Yanga, Dk. Mshindo Msolwa leo amezindua kampeni ya kuelekea mfumo wa mabadiliko ya kiuendeshaji ambayo yatakuwa chini ya kamati ndogo ya mabadiliko ya kimfumo itakayosimamiwa na Mwanasheria Alex Mgongolwa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mabadiliko hayo ambayo yanafadhiliwa na kampuni ya GSM yataifanya klabu hiyo kujiendesha katika mfumo wa kisasa ambao utakuwa unakalibisha wawekezaji na kufanya klabu hiyo kujitemea na kukua kiuchumi.

Katika zoezi hilo Mwenyekiti Msolwa ameleeza kuwa moja ya lengo lake kama kiongozi ni kubadilisha muundo wa klabu hiyo ili iweze kuingia kwenye mfumo wa kisasa tofauti na waliouzoea.

“Moja ya dhamila yangu nilivyokuwa naingia kwenye uongozi ilikuwa ni swala la kubadilisha muundo wa uendeshaji wa klabu na sasa ndoto inakalibia kutimia,” alisema Msolwa.

Awali Yanga ilimleta Carraca Antonio Domingo mtaalamu wa uendeshaji wa soka la kisasa kutoka klabu ya Benifica ya Ureno ilikuja kuwapa uzoezi katika maswala hayo ambayo kwa sasa mchakato wake unaelekea kuanza.

Yanga itakuwa klabu ya pili kuingia katika mfumo wa mabadiliko nchini baada ya watani wao klabu ya Simba kufanya hivyo kwa kutumia mfumo wa hisa ambao ambao wanachama wanaumiliki wa asilimia 51, na Mohamed Dewji ‘MO’ ambaye ni mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi anamili asilimia 49.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!