Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yazidi kuikaribia Simba, bado tatu
Michezo

Yanga yazidi kuikaribia Simba, bado tatu

Ibrahim Ajibu, mshambuliaji wa Yanga
Spread the love

YANGA imerudi nafasi ya pili baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Kagera Sugar jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hiyo ni kutokana na kufikisha pointi 43 baada ya kucheza mechi 20, sasa ikizidiwa pointi tatu tu na vinara, Simba SC.

Katika mchezo huo uliochezeshwa na Shomari Lawi kutoka Kigoma, aliyesaidiwa na Charles Simon wa Dodoma na Agnes Pantaleo wa Arusha, mabao ya Yanga yalifungwa na Ibrahim Ajib, Yussuph Mhilu na Juma Shemvuni aliyejifunga.

Baada ya dakika 45 ngumu za kipindi cha kwanza timu hizo zikimaliza bila kufungana, mvua ya mabao ikaanza kuwamiminikia Kagera Sugar kipindi cha pili.

Alianza mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Ibrahim Ajib dakika ya 53 kufunga kwa penalti baada ya beki Mzanzibari wa Kagera Sugar, Adeymum Saleh Ahmed kuunawa mpira kwenye eneo boksi.

Akafuatia winga Yussuph Mhilu kufunga la pili dakika ya 75 akimalizia majaro iliyoingizwa kwenye lango la Kagera na kiungo mshambuliaji Mzambia, Obrey Chirwa.

Zikiwa zimesalia dakika mbili mchezo kumalizika, beki wa Kagera Sugar Juma Shemvuni akamfunga kipa wake, Ramadhani Chalamanda katika harakati za kuokoa mpira uliopigwa na kiungo wa Yanga, Yusuph Mhilu aliyetokea benchi cha pili.

Katika mchezo wa leo, kiungo Mzimbabwe Thabani Scara Kamusoko alicheza kwa dakika 71 baada ya kukosekana uwanjani tangu Septemba 16, mwaka jana alipoumia kwenye mechi dhidi ya Maji Maji mjini Songea.

Mabingwa hao wa Tanzania watarudi uwanjani Jumatatu kumenyana na Stand United Uwanja wa Taifa, kabla ya kusafiri kwenda Botswana kwa mchezo wa marudiano na Township Rollers Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika, ambako wanatakiwa kushinda 2-0 waingie hatua ya makundi, baada ya kufungwa 2-1 Jumanne Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!