BAADA ya dirisha la usajiri kufungwa jana majira ya saa sita usiku, klabu ya Yanga imetoa orodha ya wachezaji tisa ambao hawatotumikia timu hiyo kwa msimu ujao wa mashindano unaotarajiwa kuanza 23, Agosti 2018. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)..
Wachazaji hao ambao ni mlinda mlango Youthe Rostand, Hassani Kessy, Yohana Mkomola, Geofrey Mwashiuya, Said Bakari, Baruani Akilimali, Said Makapu, Obrey Chirwa na Donald Ngoma.
Baadhi ya wachezaji hao wakitolewa kwa mkopo kwenda kwenye baadhi ya timu za Ligi Kuu, huku wengine wakiondoka kama wachezaji huru ambao mikataba yao imeisha toka msimu wa ligi ulipomaliza.
Mpaka sasa Yanga imeshasajili jumla ya wachezaji saba, huku wakijiandaa na mchezo wao wa marudiano dhidi ya Gor Mahia siku ya Jumapili kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Leave a comment