KIKOSI cha Yanga kimetua kwenye Uwanja wa ndege wa Bukoba mapema hii leo asubuhi tayari kwa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Kagera Sugar siku ya Jumamosi kwenye Uwanja wa Kaitaba. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kagera … (endelea).
Yanga imeondoka na kikosi chake kamili baada ya kucheza mchezo wake wa kirafiki siku ya Jana dhidi ya Mlandege Fc uliofanyika kwenye Uwanja wa Azam Complex Chamazi nakufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.
Mara baada ya kumalizika mchezo dhidi ya Kagera kikosi hiko kinatarajia kwenda mkoani Morogoro kuvaana na Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Jamhuri.
Yanga mpaka sasa imecheza michezo miwili ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kuibuka na pointi nne, mara baada ya kupata ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mbeya City na kwenda sare ya bao 1-1 mbele ya Tanzania Prisons.
Leave a comment