Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaiwahi Simba Kigoma, yapokelewa kwa shangwe
MichezoTangulizi

Yanga yaiwahi Simba Kigoma, yapokelewa kwa shangwe

Wachezaji wa Yanga wakiwasili Kigoma
Spread the love

 

KIKOSI cha klabu ya Yanga kimetua rasmi mkoani Kigoma, kwa ajili ya mchezo wa fainali wa Kombe la Shirikisho (FA) dhidi ya watani wao Simba. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Kigoma … (endelea).

Mchezo huo utapigwa kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika tarehe 25 Julai, majira ya saa 1o kamili jioni.

Yanga wamewasili Kigoma majira ya saa 1:15, kwenye Uwanja wa ndege wa Kigoma, kupitia Shirika la Ndege la Air Tanzania.

Baada ya kuwasili hapo kikosi hiko kilipokelewa na viongozi wa Yanga wakiongozwa na Kaimu Katibu Mkuu, Haji Mfikilwa, ambaye alitangulia Kigoma.

Ilipofika majira ya saa 1:35, msafara wa kikosi hiko ulitoka uwanjani hapo, huku ukilakiwa na mashabiki wao waliojitokeza kwa wingi na kuuzunguka mji wa Kigoma mpaka kuelekea Hotel ya Mwitongo ambapo kikosi hiko kimefikia hapo.

Kikosi hiko cha Yanga baadaye kitafanya mazoezi kwenye Kiwanja cha chuo cha Hali ya Hewa, Kigoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!