- WAWAKILISHI pekee katika Kombe la Shirikisho barani Afrika, Klabu ya Yanga SC imejiweka nafasi nzuri ya kutinga Fainali ya Michuano hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Marumo Gallants ya nchini Afrika Kusini. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Ni katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa nusu fainali uliopigwa leo tarehe 10 Mei 2023 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.
Kipindi cha kwanza timu zote zilikuwa zikishambualiana kwa zamu na kwenda mapumziko zikiwa hazijafungana.
Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko hata hivyo Yanga SC walinufaika na mabadiliko hayo mnamo dakika ya 64 baada ya Stephane Aziz Ki kuitanguliza Yanga Sc mbele kwa kufunga bao zuri akipokea pasi kutoka kwa Tusila Kisinda
Akitokea benchi kiungo mtukutu Benard Morrison alipigilia msumari wa pili katika dakika za jioni kabisa 90+2′ .
Timu hizo zinatarajia kurudiana katika mechi ya mkondo wa pili tarehe 17 Mei 2023 nchini Afrika Kusini.
Leave a comment