Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaizaba Marumo, yaweka mguu mmoja fainali CAFCC
Michezo

Yanga yaizaba Marumo, yaweka mguu mmoja fainali CAFCC

Spread the love
  • WAWAKILISHI pekee katika Kombe la Shirikisho barani Afrika, Klabu ya Yanga SC imejiweka nafasi nzuri ya kutinga Fainali ya Michuano hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Marumo Gallants ya nchini Afrika Kusini. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Ni katika mchezo wa mkondo wa kwanza wa  nusu fainali uliopigwa leo tarehe 10 Mei 2023 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Kipindi cha kwanza timu zote zilikuwa zikishambualiana kwa zamu na kwenda mapumziko zikiwa hazijafungana.

Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko hata hivyo Yanga SC walinufaika na mabadiliko hayo mnamo dakika ya 64 baada ya Stephane Aziz Ki kuitanguliza Yanga Sc mbele kwa kufunga bao zuri akipokea pasi kutoka kwa Tusila Kisinda

Akitokea benchi kiungo mtukutu Benard Morrison alipigilia msumari wa pili katika dakika za jioni kabisa 90+2′ .

Timu hizo zinatarajia kurudiana katika mechi ya mkondo wa pili  tarehe 17 Mei 2023 nchini Afrika Kusini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!