Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaipiga bao Simba
MichezoTangulizi

Yanga yaipiga bao Simba

Spread the love

 

MABINGWA wa kihistoria wa soka nchini Tanzania, Yanga ya jijini Dar es Salaam imeipiga bao Simba kwa kuingiza mashabiki wengi viwanjani pamoja na kujikusanyia mapato ya mlangoni. Anaripoti Junior Mitanga, TUDARCo … (endelea).

Takwimu hizo za msimu wa 2020/21, zimetolewa leo Jumatano, tarehe 22 Septemba 2021 na Bodi ya Ligi Tanzania Bara zikionesha timu za Transit Camp ikishika mkia kwenye kuingiza mashabiki wengi na kujipatia mapato kiduchu.

Msimu huo wa 2020/21, ulimalizika kwa Simba kutetea ubingwa wake mara nne mfululizo na kutetea pia ubingwa wa kombe la shirikisho.

Licha ya Yanga kutoambulia kombe lolote, lakini ilijikusanyia mapato ya mlangoni ya Sh.986.82 milioni huku Simba ikishika nafasi ya pili kwa kupata Sh.929.7 milioni. Simba na Yanga zilitumia Uwanja wa Benjamin Mkapa na Uhuru.

JKT Tanzania iliyokuwa inatumia Uwanja wa Jamhuri Dodoma imeshika nafasi ya tatu kwa kupata Sh.148.14 milioni, Dodoma Jiji Sh.139.3 milioni ambayo nayo inatumia uwanja huo huku Azam FC yenye makazi yake Chamanzi, Dar es Salaam ikishika nafasi ya 15 kati ya 20 kwa kujikusanyia mapato ya Sh.72.69 milioni.

Katika timu zilizoingiza mashabiki wengi zaidi kwenye viwanja vya nyumbani msimu wa 2020/21, Yanga imeongoza kwa kuingiza mashabiki 141,681 ikifuatiliwana watani zao Simba ikiwa na mashabiki 138,518.

Azam FC imeshika nafasi ya 17 kati ya timu 20 ikiwaimeingiza mashabiki 11,465.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!