Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yafunga mwaka kwa kishindo
Michezo

Yanga yafunga mwaka kwa kishindo

Spread the love

 

KLABU ya soka ya Yanga imefanikiwa kufunga mwaka 2021 kwa kishindo mara baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 4-0, dhidi ya Dodoma Jiji FC kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo ulipigwa hii leo tarehe 31 Desemba, 2021 kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam majira ya saa 1 usiku.

Kwenye mchezo huo ambao Yanga walitawala mpira kwa asilimia kubwa walifanikiwa kuandika bao lao la kwanza kupitia kwa Fiston Mayele kwenye dakika ya 42, na kufanya bao hilo kudumu hadi mapumziko.

Kipindi cha pili kiliporejea Yanga ilionekana kuimalika zaidi ya Dodoma Jiji na kufanikiwa kuandika bao la pili kwenye dakika ya 56 kupitia kwa Jesus Moloko mara baada ya kuunganisha mpira mrefu uliopigwa na mlinzi wao wa kati Yanick Bangala.

Mara baada ya kupata bao hilo Yanga haikuishia hapo, iliendelea kupeleka mashambulizi kwenye lango kiasi cha kupelekea mlizni wa Dodoma Jiji Justine kujifunga bao kwenye dakika ya 71 baada ya kuugusa mpira uliopigwa na Feisal Salum.

Kalamu ya mabao kwa upande wa Yanga kwenye mchezo huo ilitamatishwa na Khalid Aucho ambaye alimpigilia msumari wa bao la nne dakika ya 81.

Kwa matokeo hayo Yanga inaendelea kujikita kileleni ikiwa na alama 29, huku nafasi ya pili ikishikwa na Simba wenye alama 21 baada ya kucheza michezo tisa.

Ligi kuu hiyo itaendelea kesho kwa kupigwa mchezo kati ya Simba ambao watawalika Azam Fc kwenye dimba la Benjamin Mkapa majira ya saa 1 usiku.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!