Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaendelea kukusanya pointi, yaipiga KMC
Michezo

Yanga yaendelea kukusanya pointi, yaipiga KMC

Spread the love

 

TIMU ya Yanga ya jijini Dar es Salaam, imeendelea kuonesha makucha yake katika ligi kuu NBC Tanzania Bara 2021/22, kwa kujikusanyia pointi tatu muhimu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Ni baada ya kuutumia vyema Uwanja wa Majimaji, Songea mkoani Ruvuma leo Jumanne, tarehe 19 Oktoba 2021, kwa kuwafunga KMC FC ya Kinondoni 2-0.

Vijana hao wa Jangwani, walitumia dakika 11 za kipindi cha kwanza kujihakikishia ushindi.

Alikuwa ni Fiston Mayele dakika ya nne aliyeanza kupeleka shangwe kwa vijana hao wa Jangwani kwa kuunganisha pasi ya mwisho iliyochezwa na kiungo mahiri kwa sasa, Feisal Salum maarufu ‘Fei Toto.’

Yanga wakicheza kandanda safi na la kuvutia kwa kuliandama lango la vijana wa Kinondoni KMC, iliwachukua dakika saba baadaye yaani dakika ya 11, kwa Fei Toto kupiga shuti kali nje ya 18 na kwenda moja kwa moja langoni na kumwacha mlinda mlango Farouk Shikalo asijue la kufanya.

Kwa ushindi huo, Yanga imefikisha pointi tisa, baada ya kushinda mechi zote tatu alichoza. Alianza kwa ushindi wa 1-0 dhidi ya Kagera Sugar na Geit Gold Mine ambayo nayo alishinda 1-0.

Baada ya kutoka Songea kwenye mchezo huo ambao KMC wameutimia uwanja wa Majimaji kama wa nyumbani, Yanga watatua tena dimbani, tarehe 30 Oktoba 2021, kucheza na vijana wa Chamanzi, Azam FC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!