Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaanza kukusanya pointi Ligi Kuu
Michezo

Yanga yaanza kukusanya pointi Ligi Kuu

Spread the love

GOLI la dakika ya 86 lililofungwa kwa kichwa na beki kisiki wa Yanga, Lamine Moro limetosha kuwapa furaha mashabiki wa timu hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Ushindi huo ilioupata leo Jumapili tarehe 13 Septemba 2020 ni wa kwanza kwa mabingwa hao wa kihistoria Tanzania kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara 2020/21.

Mchezo huo umechezwa Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam ikishudia kandanda safi kutoka kwa timu zote mbili ambazo zilikuwa zikishambulia kwa zamu.

Katika mchezo wa kwanza kwenye uwanja huo, Yanga ilitoka sare ya 1-1 na Tanzania Prisons.

Mbeya City ambayo kwenye mchezo wa kwanza ilikutaka na kipigo cha 4-0 kutoka kwa KMC FC ya Dar es Salaam, mchezo uliochezwa Uwanja wa Uhuru jijini humo.

Kwa ushindi huo, Yanga imefikisha pointi nne huku Mbeya City ikicheza mchezo wa pili Dar es Salaam ikiambulia patupu.

Baada ya kumalizika kwa mchezo, Lamine Moro aliyefunga goli pekee amesema, “Namshukuru Mungu kwa kutupa ushindi. Unaweza kuona ulikuwa mchezo wenye presha ya mpira na tunamshukuru sana Mungu kwa ushindi huu.”

Moro amesema,”tumetengeneza nafasi nyingi lakini hatukufanikiwa kuzitumia zaidi ya hii moja.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!