Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga yaanza kimataifa kwa kipigo
MichezoTangulizi

Yanga yaanza kimataifa kwa kipigo

Spread the love

 

MABINGWA wa kihistoria wa soka nchini Tanzania, Yanga ya jijini Dar es Salaam wameanza vibaya safari ya michuano ya klabu bingwa Afrika kwa kukubali kipigo cha 1-0 kutoka kwa Rivers United ya Nigeria. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Yanga imeanza safari yake kwenye michuano hiyo leo Jumapili, tarehe 12 Septemba 2021, katika dimba la Benjamin Mkapa, mkoani Dar es Salaam.

Ili Yanga walioingia dimbani wakiwa na kauli mbiu ya ‘Return of the Championi’ wasonge hatua inayofuata, watalazimika kushinda mchezo wa marudiano, wiki mbili zijazo nchini Nigeria.

Goli pekee lililopeleka kilio kwa vijana hao wa Jangwani, limefungwa dakika ya 51 na Omoduemuke Moses kwa kichwa baada ya mabeki wa Yanga, kujichanganya.

Kutokana na ugonjwa wa corona, mchezo huo umechezwa bila mashabiki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

error: Content is protected !!