UONGOZI wa klabu ya Yanga umekemea vitendo vya mashabiki kuwazomea na kutokana wachezaji kiasi cha kuwakatisha tamaa na kuleta hali ya sintofahamu, licha ya klabu hiyo kupitia changamoto kadhaa kwa wakati huu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).
Yanga ambayo jana ililazimishwa sare na Azam FC, kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, na kuibuka hali ya jazba kwa upande wa mashabiki kutokana na kutovutiwa na viwango vilivyooneshwa na baadhi ya wachezaji kwenye mchezo huo.
Mashabiki wa klabu hiyo wameonekana kutupa lawama kwa washambuliaji wao David Molinga na Gnamien Yikpe kutokana na kutoonesha makali kwenye safu hiyo.
Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo imeeleza kuwa mashabiki wanapaswa kuisapoti timu yao pamoja na wachezaji ili kuleta mshikamano.
Aidha katika taarifa hiyo iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu, Wakili Simon Patrick ilieleza kuwa, klabu hiyo kwa sasa inapitia changamoto ikiwamo kutopata matokeo mazuri na mashabiki kuumia, lakini kwa sasa ni muhimu kuleta ushirikiano.
Yanga ambayo kwa sasa imeshaanza mchakato wa mabadiliko ndani ya klabu hiyo kwa kushilikiana La Liga pamoja na klabu ya Sevilla kutoka Hispania ambao wapo kama washauli.
Leave a comment