Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga wawajia juu mashabiki wao
Michezo

Yanga wawajia juu mashabiki wao

Mashabiki wa Yanga
Spread the love

UONGOZI wa klabu ya Yanga umekemea vitendo vya mashabiki kuwazomea na kutokana wachezaji kiasi cha kuwakatisha tamaa na kuleta hali ya sintofahamu, licha ya klabu hiyo kupitia changamoto kadhaa kwa wakati huu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Yanga ambayo jana ililazimishwa sare na Azam FC, kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, na kuibuka hali ya jazba kwa upande wa mashabiki kutokana na kutovutiwa na viwango vilivyooneshwa na baadhi ya wachezaji kwenye mchezo huo.

Mashabiki wa klabu hiyo wameonekana kutupa lawama kwa washambuliaji wao David Molinga na Gnamien Yikpe kutokana na kutoonesha makali kwenye safu hiyo.

Taarifa kutoka ndani ya klabu hiyo imeeleza kuwa mashabiki wanapaswa kuisapoti timu yao pamoja na wachezaji ili kuleta mshikamano.

Gnamien Yikpe

Aidha katika taarifa hiyo iliyosainiwa na Kaimu Katibu Mkuu, Wakili Simon Patrick ilieleza kuwa, klabu hiyo kwa sasa inapitia changamoto ikiwamo kutopata matokeo mazuri na mashabiki kuumia, lakini kwa sasa ni muhimu kuleta ushirikiano.

Yanga ambayo kwa sasa imeshaanza mchakato wa mabadiliko ndani ya klabu hiyo kwa kushilikiana La Liga pamoja na klabu ya Sevilla kutoka Hispania ambao wapo kama washauli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!