Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari Yanga wapewa wababe wa Kipanga kombe la Shirikisho.
HabariMichezoTangulizi

Yanga wapewa wababe wa Kipanga kombe la Shirikisho.

Spread the love

 

MARA baada ya kuangukia kwenye michuano ya kombe la Shirikisho, klabu ya soka ya Yanga imepangwa kumenyana dhidi ya Club Africain ya nchini Tunisia, katika mchezo wa mtoano. Anaripoti Damas Ndelema…(endeleaa)

 Droo ya michezo hiyo imechezeshwa hii leo tarehe 18 2022, jijini Cairo nchini Misri ambapo ndio makao makuu ya Shirikisho la Mpira Barani Afrika (CAF)

Katika mchezo huo Yanga itaanzia nyumbani kwenye dimba la Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam, tarehe 2 Novemba 2022, kwenye dimba la Benjamini Mkapa jijini Dar es Salaam, huku mchezo wa marudiano ukitarajia kupigwa nchini Tunisia tarehe 9 Novemba 2022.

Yanga imeangukia kwenye michuano hiyo, mara baada ya kuondolewa na Al Hilal ya nchini Sudan, kwa jumla ya mabao 2-1 katika michezo yote miwili.

Kwa upande wa Club Africain wao walifanikiwa kufuzu kwa hatua hii, mara baada ya kuwaondosha Kipanga ya Zanzibar kwa jumla ya mabao 7-0, katika mchezo wa marudiano huku mchezo wa kwanza uliopigwa Zanzibar Oktoba 8 mwaka huu, walitoka sare ya bila kufungana.

1 Comment

  • Mapendekezo yetu ni kuona Yanga ikishinda ila ni vigumu saana tena saana Yanga kuwashinda CLUB AFRICAIN. Club hii ni bora zaidi mara ine kuliko hata Al hilal ambayo iliwatowa Yanga week iliopita. Ila soccer ni soccer labda club yetu ya Yanga inaweza kupata nafasi kushinda michuwano yao

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!