Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Yanga waitwa Ikulu kesho Jumatatu
Michezo

Yanga waitwa Ikulu kesho Jumatatu

Spread the love
RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, kesho Jumatatu, tarehe 5 Juni 2023, ameialika Ikulu jijini Dar es Salaam, timu ya Yanga, kupata chakula cha jioni Ikulu, kwa lengo kuipongeza kwa kufanya vizuri katika michuano ya soka ya kugombea kombe la shirikisho – CAF Confederation CUP. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Katika michuano hiyo, iliyohitishwa jana jijini Algers, Algeria, Yanga waliondolewa kwa kanuni ya bao la ugenini, kufuatia ushindi wake wa bao moja kwa sifuri, kufuatia kuruhusu mabao mawili kwa moja katika mchezo wake wa kwanza jijini Dar es Salaam, wiki iliyopita.

Yanga ambayo ni mabingwa kwa mara ya pili mfululizo wa Ligi Kuu ya NBC, ilikutana na USM Alger ya Algeria, 28 Mei katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam, ambapo vijana hao wa Jangwani waliruhusu mabao hayo mawili.

Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa, imeeleza kuwa Rais Samia amewapongeza Yanga kwa kucheza vizuri katika mchezo wa pili wa fainali hapo jana kwa kuwafunga wenyeji wa mchezo huo bao 1-0 na hivyo kuwa na matokeo ya jumla ya mabao 2-2 japokuwa hawakufanikiwa kutwaa ubingwa wa kombe hilo.

Amesema, pamoja na kutotwaa ubingwa, Rais Samia anatambua kuwa Yanga wameipa heshima kubwa Tanzania na anawapongeza wachezaji, benchi la ufundi na viongozi wa timu hiyo.

Timu ya Yanga, viongozi na mashabiki wanatarajiwa kurejea nchini baadaye leo kwa ndege iliyotolewa na serikali, ikiwa ni sehemu ya Rais Samia Suluhu Hassan kuunga mkono timu hiyo iliyokuwa ikiiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!