Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga waikamua Kagera Sugar, warejea kileleni
MichezoTangulizi

Yanga waikamua Kagera Sugar, warejea kileleni

Spread the love

KLABU ya Soka la Yanga imeibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu Bara kwa kufikisha pointi 23 sawa na Azam FC lakini kukiwa na utofauti wa magoli ya kufunga. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Katika mchezo huo uliopigwa leo tarehe 13 Novemba, 2022 kwenye dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza, ulionekana kuwa mgumu kwa wachezaji wa timu zote mbili kutokana na hali mbaya ya uwanja uliokuwa umejaa maji katika baadhi ya maeneo baada ya mvua kunyesha.

Hata hivyo, Yanga walipata bao la kwanza na la ushindi, dakika ya 18 baada ya kiungo mshambuliaji kinda kutoka timu ya vijana Clement Mzize kuunganisha kwa kichwa krosi iliyochongwa na Feisal Salum.

Bao hilo lilionekana kuwaamsha wachezaji wa Kagera Sugar ambao walipeleka mashambulizi mengi ya hatari langoni mwa Yanga.

Dakika ya 70 Kagera Sugar ambao wameanza kunolewa na Meck Mexime, walipata Penalti baada ya golikipa wa Yanga kumchezea rafu Hamiss Kiiza hata hivyo Erick Mwijage alikosa Penalti iliyopanguliwa na Djugui Diarra.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!