Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Yanga kuwa vaa Kagera Sugar bila Mwamnyeto
MichezoTangulizi

Yanga kuwa vaa Kagera Sugar bila Mwamnyeto

Bakari Mwamnyeto
Spread the love

 

Klabu ya soka ya Yanga leo 29 Septemba 2021, itanza kutupa karata yake ya kwanza katika Ligi Kuu Tanzania Bara ugenini dhidi ya Kagera Sugar katika Uwanja wa  Kaitaba bila ya kuwa na nahodha wao Bakari Nondo Mwamnyeto alieye pata majeruhi mazoezi. Anaripoti Damas Ndelema TUDARCo(endelea)….. 

Mchezaji huyo ambaye pia ni nahodha wa timu hiyo amekua na kiwango kizuri kwa kutengeneza kombinesheni bora na mlinzi mwenzie wa kati Dickson Job ataukosa mchezo huu wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara kutokana na majeraha aliyoyapata akiwa mazoezi  hivyo kupelekea kukosa mchezo huu

Akizungumza  kuelekea mchezo wao wa leo dhidi ya Kagera Sugar Afisa habari wa Klabu ya Yanga Hassan Bumbuli amesema kua wachezaji wengi wote wapo vizuri kuelekea mchezo huo isipokua watamkosa nahodha wao Bakari Nondo  Mwamnyeto alipata majeruhi wakati wakiwa mazoezini hivyo kupelekea kukosa mchezo huo wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara 

“Kwenye mchezo wa leo tutamkosa nahodha wetu, Bakari Nondo Mwamnyeto ambaye alipata majeruhi kidogo katika siku mbili hizi za mazoezi, ila wachezaji wote waliobaki wapo vizuri na timamu kwa ajili ya mchezo huo, huku wakijua malengo ya klabu kwa msimu huu ni kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara”. Alisema Bumbuli

Timu hizo zitakutana huku zikiwa na kumbukumbu ya kutoka sare kwa kufungana bao 3-3 katika mchezo wao wa mwisho kukutana katika Ligi Kuu msimu uliopita katika dimba la Benjamini Mkapa Stadium jijini Dar es salaam

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!