Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa RC Chalamila: Tulipashwa kujipeleka polisi kufungwa
Habari za Siasa

RC Chalamila: Tulipashwa kujipeleka polisi kufungwa

Albert Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya
Spread the love

ALBART Chalamila, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya (RC) nchini Tanzania amesema, viongozi wa mkoa huo wamedhalilika kutokana na kumea kwa wizi wa dhahabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mbeya…(endelea).

Na kwamba, kutokana na kushindwa kusimamia madini hayo, walipaswa kujipeleka wenyewe polisi kufungwa jela walau miezi sita.

Chalamila ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 14 Desemba 2020, mbele ya Doto Biteko, Waziri wa Madini wakati wa mkutano wake na wachimbaji wadogo wa dhahabu, wadau wa madini katika Wilaya ya Chunya.

“Tulipaswa tujipeleke wenyewe polisi walau tufungwe kwa miezi sita,” amesema Chalamila akisisitiza ni aibu na fedheha kwa mkoa huo kushuhudia wizi wa madini hayo.

Hivi karibuni, kulikuwa na sakata la utoroshaji wa madini jijini humo ambalo lilihusisha polisi wawili na wafanyabishara watatu wa madini ambao tayari wamechukuliwa hatua.

Kwenye mkutano huo, Leonard Manyesha ambaye ni Mwenyekiti wa Wachimbaji Madini Mkoa wa Mbeya amesema, sababu nyingine ya wizi wa madini kushamiri Mbeya ni kutokana na utoaji holela wa leseni.

Ameshauri, utaratibu wa utoaji leseni udhibitiwe sambamba na kufanyika utafiti wa kina kwe nye migodi ya mkoa huo.

Kutokana na hali hiyo, Rais John Magufuli wakati akimwapisha Biteko hivi karibuni, alimwagiza kufuatilia suala hilo na kuchukua hatua ili kukomesha vitendo vya utoroshaji wa madini.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!