MSANII wa muziki kutoka Nigeria, Ayodeji Ibrahim Balogum ‘Wizkid’, leo ameachia Deluxe Edition ya albamu yake ya ‘’Made in Lagos.’’ Anaripoti Glory Massamu, TUDARCo … (endelea).
Wizkid katika albamu hiyo ameongeza ngoma mpya nne ambazo ni Anoti, Mood, Steady pamoja na Essence remix, aliyofanya na msanii Tems na Justine Bieber kutokea nchini Marekani.
Kabla ya Deluxe Edition, albamu hiyo ilikuwa na nyimbo 14, lakini iliyotoka sasa ina jumla ya nyimbo 18 baada ya kuongezeka nne.
Wizkid amedhibitisha kuachia albamu hiyo mpya kupitia ukurasa wake wa Instagram leo kuwa albamu hiyo imeingia sokoni rasmi leo.
Hata hivyo siku kadhaa zilizopita nyimbo ya Essence ilipata nafasi ya kupanda kwenye chati za Billboard. Lakini pia inafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya radio na televisheni duniani kote. Kusababisha mashabiki wa msanii huyo kufikiri kwamba kuna uwezekano wa Wizkid kufanya vizuri kwenye tuzo za Billboard msimu ujao.
Leave a comment