Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wizara ya Afya yamwaga ajira 1,650
Afya

Wizara ya Afya yamwaga ajira 1,650

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi
Spread the love

 

WIZARA ya Afya, imetangaza nafasi za ajira 1,650 za wataalamu wa kada mbalimbali za sekta ya afya. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Nafasi hizo zimetangazwa leo Jumamosi, tarehe 16 Aprili 2022 na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi.

“Wizara ya Afya imepata kibali cha ajira 1,650 za watalaamu wa kada mbalimbali za afya, ambao wataajiriwa na kupangiwa vituo vya kazi ambavyo vipo chini ya uendeshaji wa moja kwa moja wa Wizara ya Afya,” imesema taarifa ya Prof. Makubi.

Kwa mujibu wa taarifa ya Prof. Makubi, katika nafasi hizo, za madaktari bingwa ni 25, madaktari (215), wafamasia (15), maafisa maabara (62), wateknolojia wa dawa, maabara, mionzi na macho (155). Mafisa uuguzi (140) na maafisa uuguzi wasaidizi (467).

Nafasi nyingi ni, wauguzi (140), wakemia (2), madaktari wa afya ya kinywa na meno (15), tabibu meno (19), watoa tiba kwa vitendo (15), wazoeza viungo kwa vitendo (31), maafisa wazoeza viungo (33), maafisa afya mazingira (40), wahandisi vifaa tiba (17), wateknolojia vita tiba (40), watunza kumbukumbu wa afya (10) na madereva (4).

Taarifa ya Prof. Makubi imesema, waombaji watakaochaguliwa watapangiwa kazi kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa wa wataalamu wa kada za afya na hakutakuwa na kubadilisha kituo cha kazi ndani ya miaka mitatu.

Mikoa iliyotajwa kuwa ina upungufu huo na Prof. Makubi ni pamoja na, Kigoma, Katavi, Sumbawanga, Songwe, Njombe, Ruvuma, Mtwara, Lindi, Simiyu, Geita, Mara, Hospitali za Kanda za Chato na Mtwara, Hospitali ya Magonjwa Ambukizi Kibong’oto na vyuo vya afya.

Taarifa ya Prof. Makubi imesema, maombi hayo yatumwe ndani ya wiki mbili kuanzia leo.

Kwa undani wa Taarifa hiyo ya ajira za Wizara ya Afya ingia HAPA

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!