BENKI ya NMB nchini Tanzania imetoa T-shirt 800 kwa Wizara ya Fedha na Mipango kwa ajili ya wiki ya Manunuzi ya Umma nchini humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).
Wiki hiyo ya manunuzi yenye kauli mbiu ya ‘Matumizi ya teknolojia katika kubiresha ununuzi wa umma’ imezinduliwa leo Alhamisi tarehe 5-7 Mei 2022 na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa jijini Arusha.
T-shirt hizo zimekabidhiwa na Meneja wa NMB Kanda ya Kaskazini, Dismas Prosper kwa Afisa Ugavi Wizara ya Fedha na Mipango, Hilda Segere.
Aidha, kwenye makabidhiano hayo alikuwepo Meneja wa Benki ya NMB Tawi la Clock tower, Emmanuel Kishosha.
Leave a comment