Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa WHO yatangaza kumalizika Ebola DRC
Kimataifa

WHO yatangaza kumalizika Ebola DRC

Spread the love

 

SHIRIKA la Afya Ulimwenguni (WHO) limesema mlipuko wa hivi punde wa Ebola umedhibitiwa ndani ya miezi mitatu kutokana na “mwitikio wa haraka” na “madhubuti” katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Anaripoti Mwandishi Wetu kwa msaada wa mashirika ya kimataifa … (endelea).

Kwa mujibu wa Shirika la Utangazaji la BBC watu wanne wamefariki tangu mlipuko huo wa 14 nchini humo tangu 1976 kutangazwa mwezi Aprili katika mji wa magharibi wa Mbandaka.

Watatu kati ya waliokufa walichukuliwa kuwa “kesi zilizothibitishwa” na mmoja alichukuliwa kuwa kesi shirika la afya ulimwenguni lilisema.

Shirika la Umoja wa Mataifa lilifanya kazi pamoja na serikali kusambaza chanjo, upimaji, ufuatiliaji,kuzuia na kudhibiti maambukizi, pamoja na ushirikishwaji wa jamii.

“Matokeo haya yanaonyesha kuimarisha utayari, ufuatiliaji wa magonjwa na ugunduzi wa haraka, kupiga hatua mbele,” Mkurugenzi wa WHO Kanda ya Afrika Dk Matshidiso Moeti alisema katika taarifa yake Jumatatu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!