Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa WB kuitosa Tanzania? Kikao cha dharura chafanyika
Habari za SiasaTangulizi

WB kuitosa Tanzania? Kikao cha dharura chafanyika

Spread the love
MSIMAMO wa Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo na Asasi za Haki za Binadamu za Kimataifa nchini Tanzania, umeisukuma Bodi ya Wakurugenzi ya Benki ya Dunia (WB), kuahirisha kikao chake. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kikao hicho cha kujadili hatma ya kuipa fedha za mkopo Serikali ya Tanzania, zaidi ya Dola za Marekani milioni 500, kilipangwa kufanyika leo tarehe 28 Januari 2020, lakini kimeahirishwa baada ya WB kufanya kikao cha dharura na wanaharakati pia asasi za kiraia nchini.

Katika barua ya Zitto kwa WB, aliitaka taasisi hiyo kutotoa fedha hizo, zilizopangwa kuboresha sekta ya elimu nchini kwa madai, serikali ya Rais John Magufuli, imeshindwa kuheshimu utawala wa sheria na haki za binadamu pamoja na kuzuia wanafunzi wa kike wanaopata ujauzito wakiwa shuleni, kuendelea na masomo.

“Mkopo wa Benki ya Dunia utalipwa na kila Mtanzania. Serikali lazima iweke mazingira ya watoto wa kike kupata elimu bila kubaguliwa.

“Watoto waliopata uja uzito shuleni, wawe na fursa kurejea shuleni bila bugudha wala unyanyapaa. Badala ya kulia lia, rekebisheni mkataba wa mkopo,” aliandika Zitto kupitia ukurasa wake wa twitter tarehe 26 Januari 2020.

Kwa mujibu wa mtandao wa CNN, katika kikao hicho cha dharura WB, mjumbe mmoja wa bodi hiyo aliomba kikao hicho kiahirishwe.

Wiki iliyopita, WB ilitoa taarifa kwamba, itafanya kikao cha kujadili sababu zilizotolewa na wanaharakati hao, juu ya kutoipa mkopo huo serikali ya Tanzania.

Miongoni mwa sababu zilizotolewa na wanaharakati hao, ni wanafunzi wanaopata ujauzito wakiwa shuleni, kuzuiwa kuendelea na masomo kinyume na haki za binadamu, pamoja na ukiukwaji mwingine wa haki za binadamu na utawala bora.

Licha ya tuhuma zinazoelekezwa kwa Rais Magufuli, Bella Bird, Mkurugenzi Mkazi wa WB nchini Tanzania ambaye anatarajiwa kuachia ofisi hiyo Ijumaa wiki hii, kwenye kikao hicho cha dharura aliwaeleza wanaharakati hao sababu za timu yake kupendekeza mkopo huo utolewe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!