Saturday , 9 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Waziri Ummy atoa sababu kusitisha taarifa za corona
Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atoa sababu kusitisha taarifa za corona

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imesema imesimama kutoa takwimu za mwenendo wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na virusi vya corona (COVID-19), kwa sababu ya matatizo ya kiufundi yaliyojitokeza katika maabara inayopima ugonjwa huo. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Sababu hiyo imetolewa leo Ijumaa tarehe 8 Mei 2020 na Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya wa Tanzania, ikiwa zimepita siku tisa tangu Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu, kutangaza ongezeko la wagonjwa wapya 196 wa COVID-19.

Waziri Ummy amesema Serikali itatoa takwimu za mwenendo kuhusu ugonjwa huo, pindi maboresho ya kiufundi katika Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii, yatakapokamilika.

Aidha, Waziri Ummy amewatoa hofu wananchi juu ya ukimya huo, akisema maboresho hayo yatakamilika ndani ya muda mchache.

https://www.youtube.com/watch?v=DACBK6Q0S_c

“Takribani siku saba sasa hatukuweza kutoa taarifa za takwimu za maabara  kuhusu mwenendo wa corona nchini,  kwa sababu sasa hivi tunafanya maboresho  ya  maabara ya taifa ya afya ya jamii.”

“Hivyo niwatoe hofu wananchi kwamba ndani ya siku chache zoezi litakamilika, na tutaendelea kutoa taarifa kwa umma mara kwa mara,” amesema Waziri Ummy.

Kauli hiyo ya Waziri Ummy ameitoa ikiwa ni siku tano tangu alipomwelekeza Katibu Mkuu Wizara ya Afya kuwasimamisha kazi mkurugenzi wa Maabara ya Taifa ya Afya ya Jamii, Dk. Nyambura Moreni na Jacob Lusekelo, Meneja Udhibiti wa Ubora ili kupisha uchunguzi.

Uamuzi huo wa Waziri Ummy ulikwenda sambamba na kuunda kamati ya wataalamu wa afya yenye watu kumi inayoongozwa na Profesa Eligius Lyamuya wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS).

Kamati hiyo inapaswa kukabidhi ripoti kwa Waziri Ummy, tarehe 13 Mei 2020.

Waziri Ummy alitoa maagizo hayo ikiwa ni siku moja kupita tangu Rais wa Tanzania, John Magufuli kubainisha changamoto mbalimbali kwa maabara hiyo ikiwamo kupima vitu mbalimbali ikiwamo mapapai na mbuzi na kukutwa na corona hali aliyodai inaonyesha hakuna umakini katika maabara hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

Habari Mchanganyiko

Tanesco: Mvua chanzo kukatika umeme leo

Spread the loveShirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limedai kuwa hitilafu iliyojitokeza katika...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Zara tours yajivunia kupandisha wageni 228 Mlima Kilimanjaro

Spread the loveKampuni ya utalii ya Zara tours ya mjini Moshi mkoani...

error: Content is protected !!