Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri Ummy alipia mashabiki 1000 Coastal, wachezaji awaahidi…
Habari za Siasa

Waziri Ummy alipia mashabiki 1000 Coastal, wachezaji awaahidi…

Spread the love

 

WAZIRI Ofisi ya Rais-Tamisemi, Ummy Mwalimu amewaahidi Sh.5 milioni, wachezaji wa Coastal Union endapo watafanikiwa kubaki Ligi Kuu Tanzania bara huku akilipia tiketi za mashabiki 1,000. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tanga…(endelea).

Coastal Union inashika Uwanja wa Mkwakwani Tanga leo Jumamosi, tarehe 24 Julai 2021, kucheza na Pamba ya jijini Mwanza, kuwania kusalia au kupanda Ligi Kuu.

Katika mchezo wa awali uliochezwa Mwanza, timu hizo zilimaliza dakika 90 kwa kufungana 2-2.

Leo asubuhi, Ummy ambaye ni Mbunge wa Tanga Mjini (CCM), ametembelea kambi ya wachezaji wa Coastal Union ambapo amezungumza nao na kuwaahidi kitita hicho cha fedha ikiwa ni kuwatia moyo.

Kuhusu tiketi hizo za bure, Waziri Ummy amesema, zitapatikana milangoni Mkwakwani na Ofisi ya Mbunge wa Tanga Mjini kuanzia saa 5 asubuhi.

Mchezo mwingine unapigwa Uwanja wa Jamhuri Morogoro kati ya Mtibwa Sugar dhidi Transit Camp.

Katika mchezo wa awali ulipigwa Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, Mtibwa iliibuka na ushindi mnono wa 4-1.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!